Joshua Kiziba
Rais aelekeza fedha za sherehe za Muungano zitumike kwenye shughuli za maendeleo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza fedha zilizokuwa zimepangwa kugharamia maadhimisho ya Sherehe za Muungano mwaka huu, zitumike kwenye shughuli za maendeleo, ikiwemo kukarabati miundombinu ya barabara iliyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.
Hayo yameelezwa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchembaleo ofisini kwake Mlimwa jijini Dodoma alipokuwa akiuarifu umma kuhusu maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanzania yatakavyofanyika.
“Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Muungano yatafanyika katika ngazi ya mikoa yote nchini ambapo viongozi wakuu wa kitaifa watafanya shughuli za kutembelea, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi ya maendeleo,” amesema Dkt. Mwigulu.
Aidha, amesema imeelekezwa kuwa wakuu wa mikoa watembelee, waweke mawe ya msingi na kuzindua miradi ya maendeleo pamoja na kushiriki shughuli za usafi wa mazingira, kupanda miti na kufanya mashindano ya michezo mbalimbali.
Shughuli nyingine zitakazoambatana na maadhimisho hayo ni mashindano ya michezo na sanaa mbalimbali, mashindano ya uandishi wa insha kwa shule za msingi na sekondari, mahojiano maalum na wazee maarufu, midahalo na makongamano kuhusu muungano na hatua ya maendeleo iliyofikiwa hadi sasa.
Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni: “MIAKA 62 YA MUUNGANO: AMANI, UMOJA NA MSHIKAMANO NI MSINGI WA MAENDELEO ENDELEVU.”
Bugando yaandika historia kwa kufanya upandikizaji wa figo kwa mara ya kwanza
Mwanza: Kwa mara ya kwanza katika historia yake, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando imefanikiwa kufanya upasuaji wa upandikizaji figo, hatua inayofungua ukurasa mpya wa huduma za kibingwa bobezi kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa.
Upasuaji huo wa mafanikio umefanyika kwa mgonjwa mwenye umri wa miaka 40 (mwanaume), mkazi wa Mkoa wa Mwanza, kwa ushirikiano wa karibu kati ya wataalamu wa Hospitali ya Bugando na timu ya wataalamu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando, Sr. Dkt Alicia Massenga, amesema hatua hiyo ni mafanikio makubwa kwa sekta ya afya nchini, na serikali kwa ujumla.
“Leo Bugando imeandika historia, kuanzishwa kwa huduma hii ya upandikizaji figo ni mkombozi kwa maelfu ya wananchi wa kanda hii, maandalizi yalikua ya muda mrefu lakini leo hii tumefanikiwa kufanikisha zoezi hili,” amesema.
Sr. Massenga ameongeza kuwa mafanikio hayo yametokana na uwekezaji kwa ushirikiano wa Baraza la Maaskofu (TEC) na Serikali katika miundombinu, vifaa, na mafunzo kwa wataalamu.
“Huu ni uthibitisho kuwa ushirikiano baina ya hospitali hizi unaokoa maisha ya Watanzania. Tunakusudia kufanya upandikizaji kwa wagonjwa wengine hapa Bugando kuanzia sasa, tunawakaribisha sana kwa huduma hii,” ameongeza.
Kwa upande wake kiongozi wa timu kutoka Benjamini Mkapa, Prof. Masumbuko Mwashambwa, Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka UDOM na pia kiongozi wa timu ya upandikizaji figo katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma akiiwakilisha Timu hii ya wataalamu amesema, wapo tayari kuendelea kushirikiana na Bugando wakati wote.
Serikali imeweka kipaumbele kikubwa katika ajira katika mwaka 2026/27, ambapo jumla ya nafasi mpya 45,000 zinatarajiwa kujazwa ili kupunguza upungufu wa watumishi katika taasisi mbalimbali za umma.
Sambamba na hilo, vibali vya ajira mbadala 7,124 vitatolewa kuhakikisha utendaji kazi haukwami pindi watumishi wanapoondoka kazini kwa sababu mbalimbali.
Katika kulinda haki za watumishi, serikali imepanga kuhakiki na kuidhinisha madai ya malimbikizo ya mishahara katika taasisi 425, pamoja na kushughulikia madai ya wastaafu na waliokoma utumishi kutoka kwa waajiri 200. Pia, usimamizi wa malipo ya mishahara utaimarishwa katika taasisi 510 ili kuhakikisha malipo yanafanyika kwa wakati na kwa usahihi.
Kwa upande wa maboresho ya mifumo ya kiutumishi, serikali itafanya uhakiki wa watumishi (staff audit) katika taasisi 127 zinazotumia mfumo wa e-Watumishi, huku taasisi 35 ambazo bado hazijaanza kutumia mfumo huo zitawezeshwa kujiunga nao. Maboresho zaidi yatahusisha kuimarisha teknolojia ya mfumo huo na kuunganisha na mifumo mingine ya serikali pamoja na sekta binafsi.
Aidha, serikali imepanga kuanzisha mfumo maalum wa “dashboard” utakaokusanya na kuwasilisha takwimu sahihi kutoka mifumo mbalimbali ikiwemo e-Watumishi, e-Msawazo, e-Utendaji na Watumishi Portal, hatua inayotarajiwa kuboresha maamuzi ya kiutendaji katika ngazi zote za serikali.
Mpango huo unaonesha dhamira ya serikali ya kuendelea kuboresha utumishi wa umma kwa kuweka mifumo madhubuti, kuongeza ajira na kuhakikisha watumishi wanapata stahiki zao kwa wakati.
Tanzania to finalise Public Investment Bill to boost state entities’ efficiency
Dodoma. The government has said it will finalise the Public Investment Bill in the 2026/27 financial year as part of reforms aimed at improving the performance of public entities and strengthening their contribution to Dira 2050.
Presenting the 2026/27 budget estimates for the Ministry of State in the President’s Office (Planning and Investment), the responsible minister, Prof Kitila Mkumbo, said the Bill will provide a legal framework for managing public investments, focusing on efficiency, accountability and improved performance of state entities.
He said it will propose establishing a Public Investment Management Authority to coordinate government investments within a unified framework.
The Bill will also propose a Public Investment Fund to mobilise capital for investments through state-owned entities without affecting contributions to the Consolidated Fund. On governance, the Bill will introduce competitive recruitment for chief executives and boards of public institutions to improve professionalism and accountability.
It will also grant greater operational autonomy to commercial state-owned enterprises while strengthening performance-monitoring systems.
Prof Mkumbo said the reforms aim to reduce reliance on government subsidies and improve efficiency in public entities.
The Office of the Treasury Registrar oversees 308 entities, including 91 commercial institutions, with total investments valued at Sh92.3 trillion.
The government will continue reviewing public entities, including merging those with overlapping functions and dissolving those no longer relevant.
Following a 2023 review, 14 entities were merged and three dissolved. TIC and EPZA were also merged to form TISEZA.
Prof Mkumbo said further mergers are being finalised.
Non-tax revenue from public entities is projected at Sh1.79 trillion in 2026/27, up from Sh1.69 trillion.
The reforms aim to increase the contribution of public entities to up to 8 per cent of GDP by 2050.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa tuzo maalum ya Ubinadamu ya Upasuaji wa Ubongo kutokana na mchango wake mkubwa katika kuimarisha sekta ya afya nchini.
Tuzo hiyo imetolewa leo na Rais wa Chama cha Madaktari wa Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu Tanzania, Dkt. Othman W. Kiloloma katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Jumuiya ya Madaktari wa Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) alioufungua jijini Dar es Salaam.
“Kwa niaba ya chama cha wataalam wa upasuaji wa ubongo na mgongo tunakutambua na kukushukuru kwa mchango wako mkubwa wa ubinadamu, ni heshima yangu kubwa kukukabidhi tuzo ya ubinadamu ya upasuaji wa ubongo, hongera sana,” amesema Dkt. Kiloloma.
Amesema kuwa, kupitia uwekezaji uliowekwa na Serikali ya awamu ya sita katika huduma za kibingwa na ubingwa bobezi, ujenzi wa rasilimali watu na uimarishaji wa huduma za vipimo, dharura na bima ya afya kwa wote umeokoa maisha na matumaini ya maisha ambayo wengine hawakuwa nayo.
Akizungumza Rais Samia amesema katika miaka mitano iliyopita kazi kubwa iliyofanyika imeleta matokeo ambapo hospitali zinazofanya upasuaji wa kibingwa wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu zimeongezeka kutoka 2 hadi 7, madaktari bingwa wa upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu wameongezeka kutoka 12 hadi 37, na serikali imeongeza kwa kiasi kikubwa vifaa muhimu kama MRI, CT-Scan na X-ray.
Aidha, amesema tuzo huyo ni heshima kwa Watanzania wote na ameahidi kuwa serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za kikanda na kimataifa kuimarisha huduma za afya kwa kuzifanya kuwa bora, nafuu na za uhakika ili kuokoa maisha ya wananchi na kurejesha tumaini kwa jamii.
Chwakwera delivers Commonwealth’s message to Samia as envoy concludes working visit
Dar es Salaam: President Samia Suluhu Hassan, on Wednesday, April 15, 2026, received a special message from the Secretary General of the Commonwealth of Nations, Shirley Ayorkor Botchwey, delivered by the organisation’s Special Envoy and former Malawi President, Lazarus McCarthy Chakwera, at State House in Dar es Salaam.
The message outlined priority areas under the Commonwealth’s engagement with Tanzania, including transparency and cooperation in assessing developments during and after the 2025 General Election.
The statement said the engagement also focuses on enhancing political participation, advancing inter-party dialogue and strengthening institutional accountability.
In the message, Ms Botchwey reaffirmed the Commonwealth’s commitment to continued engagement with Tanzania to reinforce democratic governance, the rule of law and national reconciliation following developments surrounding the October 2025 polls.
“She noted that the Commonwealth supports ongoing efforts in the country and stands ready to assist in fostering a stable, inclusive and credible political environment through dialogue and institutional reforms,” the statement said.
During the meeting, President Hassan said Tanzania is addressing the situation through its national institutions, citing measures undertaken by the government, including the establishment of an independent Commission of Inquiry aimed at restoring stability and enhancing accountability.
She said the findings of the commission will inform subsequent actions, including accountability processes, reconciliation efforts and institutional reforms, while the government continues to facilitate dialogue through legally established platforms and broader stakeholder engagement.
For his part, Dr Chakwera reiterated the Commonwealth’s readiness to work with Tanzania in advancing the rule of law, political cooperation and national cohesion.
Dr Chakwera concluded his working visit to Tanzania in his capacity as Special Envoy of the Commonwealth Secretary-General to assess the political environment and reconciliation efforts, during which he held consultations with a range of political and institutional stakeholders.
